WATU 19 wakiwemo abiria na wahudumu wamefariki dunia katika ajali ya ndege ya shirika la Ndege la Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Jumapili tarehe 6 Novemba, 2022 katika Ziwa Victoria Mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza vifo vya watu 19 wakiwemo abiria na wahudumu katika ajali ya ndege ya shirika la Ndege la Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Jumapili tarehe 6 Novemba , 2022 katika Ziwa Victoria Mkoani Kagera.
Majaliwa ametangaza vifo hivyo leo jioni ikiwa ni saa chache baada ya kuwasili kwenye eneo ilipotokea ajali hiyo.
Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa huo, Albert Chalamila, ndege hiyo Precision Air ATR 42 SH PWF ilikuwa na watu 43, kati yao 39 wakiwa abiria, marubani wawili na wahudumu wawili ambapo tayari 28 wameokolewa.
Taarifa hiyo ya Waziri Mkuu imekuja ikiwa ni saa chache baada ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Issessanda Kaniki kuthibitisha kutokea kwa vifo vya watu watatu.
Leave a comment