Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 19 wafariki dunia ajali ya ndege Bukoba
Habari MchanganyikoTangulizi

19 wafariki dunia ajali ya ndege Bukoba

Spread the love

WATU 19 wakiwemo abiria na wahudumu wamefariki dunia katika ajali ya ndege ya shirika la Ndege la Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Jumapili tarehe 6 Novemba, 2022 katika Ziwa Victoria Mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza vifo vya watu 19 wakiwemo abiria na wahudumu katika ajali ya ndege ya shirika la Ndege la Precision Air iliyotokea asubuhi ya leo Jumapili tarehe 6 Novemba , 2022 katika Ziwa Victoria Mkoani Kagera.

Majaliwa ametangaza vifo hivyo leo jioni ikiwa ni saa chache baada ya kuwasili kwenye eneo ilipotokea ajali hiyo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa huo, Albert Chalamila, ndege hiyo Precision Air ATR 42 SH PWF ilikuwa na watu 43, kati yao 39 wakiwa abiria, marubani wawili na wahudumu wawili ambapo tayari 28 wameokolewa.

Taarifa hiyo ya Waziri Mkuu imekuja ikiwa ni saa chache baada ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Issessanda Kaniki kuthibitisha kutokea kwa vifo vya watu watatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!