Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 158,000 waomba ajira 17,000, Serikali yaongeza siku 4
Habari Mchanganyiko

158,000 waomba ajira 17,000, Serikali yaongeza siku 4

Innocent Bashungwa
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imeongeza siku nne zaidi kwa waombaji wa ajira za ualimu na afya kutoka jana Jumatano tarehe 4 hadi 8 Mei 2022, saa 5:59 usiku. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa amesema hatua ya kuongeza siku hizo ni kutoa fursa kwa walioshindwa kuomba maombi hayo tangu zilipotangazwa 20 Mei 2022.

Amesema mpaka kufikia juzi Jumanne tarehe 3 Mei 2022 saa 5:59 usiku, waombaji waliowasilisha maombi kupitia mfumo wa kada ya afya ni 39,053 na kada ya elimu ni 119,133 hivyo jumla ya waombaji wote wakiwa 158,186.

Waziri Bashungwa amesema, Tamisemi ilipata kibali cha ajira za watumishi 9,800 kwa kada ya ualimu na 7,612 kwa kada ya afya ambapo ajira zote ni 17,412.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!