Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo 14 za fuzu makundi kombe la Shirikisho Afrika
Michezo

14 za fuzu makundi kombe la Shirikisho Afrika

Spread the love

 

JUMLA ya Timu 14, kati ya 16 zimefanikiwa kufuzu kwa hatua ya makundi ya michuano ya kombe la Shirikisho Barani Afrika, mara baada ya kushinda michezo yao ya mtoano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu….(endelea)

Michezo hiyo ya marudiano ilipigwa jana Jumapili, tarehe 5, Disemba 2021, katika viwanja mbalimbali.

Timu ya kwanza kufuzu katika hatua hiyo ilikuwa ni Simba ambao wal;ishuka dimbani mapema majira ya saa 10, ugenini kumenyana na Red Arrows ya nchini Zambia na kupoteza mchezo huo kwa mabao 2-1, lakini walifanikiwa kufuzu kutokana na kuwa uwiano mzuri wa mabao.

Simba ilifuzu hatua hiyo kwa jumla ya mabao 4-2, katika michezo yote miwili, mchezo wa kwanza ulipigwa Dar es Salaam, tarehe 28, Novemba 2021 Simba ilifanikiwa kuondoka na ushindi wa mabao 3-0.

Klabu zingine ambazo zimefuzu kwenye hatua hiyo ya makundi ni pamoja na As Otoho na TP Mazembe kutoka nchini Congo, Coton sport ya Cameroon, Asec Mimosas, Orlando pirates kutoka Afrika Kusini, US Gendarmerie ambao wamefuzu kwa mara ya kwanza.

Wengine ni Al Masry sc, Pyramids zote kutoka Misri, Zanaco ya Zambia, Js saoura, Cs Sfaxien kutokaTunisia, Ahly Tripoli ya Libya na RS Berkane kutoka nchini Morocco.

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!