Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 12 waibuka washindi NMB bonge la Mpango
Habari Mchanganyiko

12 waibuka washindi NMB bonge la Mpango

Spread the love

 

NAKAUNDA Mangosongo na Charles Mkwizu ambao ni wakazi wa Dodoma wamejishindia pikipiki za miguu mitatu aina ya Sky Mark katika droo ya kwanza ‘NMB Bonge la Mpango – 2merudi Tena.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Droo hiyo ilichezeshwa jana Jumatano, tarehe 13 Machi 2021 ya shindano hilo awamu ya pili ya kampeni ya weka akiba na ushinde inayoendeshwa na benki hiyo.

Mbali na Mangosongo na Mkwizu, washindi wengine 10 waliojinyakulia fedha taslimu Sh.100,000 ni: Kuluthum Chande, George Fabiano, Justine Yona, Justina Mbuya na Beatrice Tarimo.

Pia, wamo Gloriana Nicholaus, Paschal Phabian, Alphonce Donatus, Ramadhani Khalfan, Kelvin Mosha.

Akizungumza kabla ya kuchezeshwa kwa droo hiyo, Meneja Mwandamizi wa Idara ya Wateja Binafsi wa NMB, Ally Ngingite, alisema katika kipindi chote cha kampeni hiyo ya wiki 12, zawadi zote zenye thamani ya Sh.237 milioni zitaenda kwa washindi 170, ambao wataweka akiba katika akaunti ama kufungua akaunti mpya zenye akiba isiyopungua Sh.100,000.

“Kila wiki tutakuwa na droo za kupata washindi 12, wakiwemo 10 wa pesa taslimu Sh.100,0000 kila mmoja huku wengine wawili wakijishindia pikipiki za miguu mitatu (moja kwa kila mmoja), aina ya Sky Mark yenye thamani ya Sh.4.5 milioni.”

Ngingite aliwaomba wateja wa benki hiyo kuendelea kujiwekea akiba ili kujiongezea nafasi ya kushinda fedha taslimu ama pikipiki.

“Na kwa wale wasio na akaunti, watembelee matawi yetu yaliyotapakaa kote nchini, waweze kufungua akaunti na kuweka akiba angalau ya Sh laki moja, waingie kwenye droo hizi na kushinda,” alisema Ngingite.

Droo hiyo ilichezeshwa mbele ya afisa toka Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT), Joram Mtafya, ambaye aliwahakikishia Watanzania kuwa kampeni hiyo itafanyika kwa kufuata sheria na kanuni zinazosimamia michezo hiyo na kwamba, hata akaunti za watoto walio chini ya umri wa miaka 18 (zinazoendeshwa na wazazi ama walezi), zinaweza kushinda zawadi hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!