Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto ‘udenda’ wamtoka urais 2020
Habari za Siasa

Zitto ‘udenda’ wamtoka urais 2020

Spread the love
ZIITO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema, yupo tayari kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

 “Mimi napenda kuwa rais lakini ni suala la mazingira ya muktadha wa nchi wa sasa. Na kama wenzangu wataona kwa mazingira ya sasa Zitto anafaa kupambana na CCM, sitaukimbia msalaba huo,” amesema Zitto.

Amesema, hatua hiyo itafikiwa endapo muungano wa vyama wanaotarajia kuufuanya, utampa ridhaa hiyo.

Wakati akitoa kauli hiyo, Maalim Seif Sharif Hamada ambaye ni Mshauri Mkuu wa chama amesema, yupo tayari kugombea urais viziwani Zanzibar kwenye uchaguzi huo.

Wakizungumza katika mkutano na wanahabari leo tarehe 31 Desemba 2019, jijini Dar es Salaam kila mmoja amesema, watagombea nafasi hizo pale watakapoteuliwa kugombea.

Maalim Sief ameeleza kuwa, kwa sasa hana uhakika kama atagombea urais Zanzibar, lakini kama chama chake na Wazanzibari watampa ridhaa, atagombea.

“Mimi sijakata shauri kama nigombee au nisigombee, nategemea mazingira hayo,” amesema Maalim Seif ambaye amewahakikishia wafuasi wa chama hicho kwamba CCM itanag’olewa kwenye uchaguzi huo.

Akifafanua dhamira yake ya urais, Zitto amesema ndoto yake ni kuwa Rais wa Tanzania, na kwamba kama chama chake kitamteua kugombea nafasi hiyo kwenye uchaguzi mkuu wa 2020, atagombea.

“Ningependa kushiriki kwa dhati kuleta mabadiliko ambayo Watanzania wanapaswa kuwa nayo. Sasa hivi si suala la nani anakuwa mgombea.

“Ni jambo ambalo lazima wadau wote wanaotaka kuing’oa CCM madarakani. Inatakiwa kuangalia nani  na kwa mazingira haya anafaa kubeba bendera ya kuiondoa,” amesema Zitto.

Amesema, anaumizwa na wimbi la umasiki linalowakabili Watanzania wengi, na kuahidi kwamba endapo atapata ridhaa ya kuwa Rais wa Tanzania, ataweka sera rafiki zitakazoleta maendeleo ya Watanzania.

“Mimi bianfsi naumizwa sana na hali ya maendeleo ya nchi yetu, naumizwa na ugumu wa maisha wananchi wanayopitia. Ugumu ambao haujasababisha na Mungu umesababishwa na sera fyongo za CCM. Ugumu huu wa maisha hatukustahili,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!