Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto azidi kusota na safari za Polisi Dar
Habari za SiasaTangulizi

Zitto azidi kusota na safari za Polisi Dar

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo akizungumza na waandishi wa Habari muda mchache baada ya kutoka kuripoti Kituo cha Polisi Chang'ombe, Dar es Salaam
Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameendelea kusota na safari za kwenda kuripoti katika kituo cha polisi cha Chang’ombe jijini Dar es Salaam, anaandika Hamis Mguta.

Kwa mara nyingine Zitto leo asubuhi ameripoti tena polisi siku ambayo wajumbe wa kamati kuu ya chama hicho nao wamefika katika polisi katika kitengo cha makosa ya fedha kwa ajili mahojiano kuhusu takwimu za uchumi.

Takwimu hizo zilitolewa na chama hicho hivi karibuni hatua ambayo imewaweka matatani.

“Nimeripoti na nimetakiwa kufika tena tarehe 17 mwezi huu, mahakama ndio itakayotoa tafsiri ya hili kwa sababu kuna wanasheria,” amesema Zitto.

Aidha, amesema kuwa chama kinaamini walichokifanya ni sahihi kwa kuwa walichokifanya ni kutafsiri na kuchambua takwimu zinazotolewa na ofisi ya taifa ya takwimu na hawakuongeza jambo.

Kadhia hii inahusisha baadhi ya maneno katika hotuba yake ya Oktoba 29, 2017 alipokuwa kwenye mkutano wa kuzindua kampeni za udiwani katika Kata ya Kijichi, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.

Moja ya matamshi yaliyomuweka Zitto matatani ni pamoja na kusema kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu serikali yake imeshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku hiyo.

Kadhalika Zitto anadaiwa kuwataka wananchi wasiichague CCM kwa sababu serikali yake imeshindwa kueleza chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach.

Hivyo Zitto akasema kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.

Zitto aliongozana na timu ya wakili wa chama pamoja na mke wake katika kituo hicho cha Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Baada ya kutoka kituoni hapo alielekea kituo Kituo cha Polisi Kamata, ambapo kaimu Mwenyekiti wa Chama, Yeremiah Maganja, pamoja na Katibu Mkuu, ndugu Dorothy Semu, wameitikia wito wa Kamishna wa Makosa ya Jinai (DCI) wa Jeshi la Polisi kituoni hapo ambapo hadi sasa bado wanaendelea na mahojiano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!