Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto afungua kesi kupinga muswada, yahairishwa mpaka mchana
Habari za SiasaTangulizi

Zitto afungua kesi kupinga muswada, yahairishwa mpaka mchana

Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzake wawili, Joran Bashange na Salim Bimani wamefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa imehairishwa hadi leo saa nane mchana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kesi hiyo imefunguliwa leo katika Mahakama Kuu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupingaMuswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa na kuzuia usijadiliwe bungeni mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa.

Kwa mujibu wa Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, ACT Wazalendo, kesi hiyo imehairishwa mpaka saa nane ambapo Mahakama Kuu itaamua kuhusu hoja kuu mbili zilizozua ubishani mkubwa wa hoja baina ya upande wa wanasheria wa waombaji (Applicants) na upande wa Mwanasheria Mkuu wa serikali.

Hoja zilizoibua mvutano ni upande wa muda wa Mwanasheria Mkuu wa serikali kujibu hoja zilizoibuliwa na waombaji uongezwe kama ilivyoombwa na upande wa AG au upunguzwe kama ilivyoombwa na upande wa waombaji.

Pia kama Mahakama iweke zuio (Injunction) la kuzuia muswada kujadiliwa Bungeni, kama ilivyoombwa na waombaji mpaka kesi ya msingi itaposikilizwa na kuamuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!