KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzake wawili, Joran Bashange na Salim Bimani wamefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa imehairishwa hadi leo saa nane mchana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Kesi hiyo imefunguliwa leo katika Mahakama Kuu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupingaMuswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa na kuzuia usijadiliwe bungeni mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa.
Kwa mujibu wa Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, ACT Wazalendo, kesi hiyo imehairishwa mpaka saa nane ambapo Mahakama Kuu itaamua kuhusu hoja kuu mbili zilizozua ubishani mkubwa wa hoja baina ya upande wa wanasheria wa waombaji (Applicants) na upande wa Mwanasheria Mkuu wa serikali.
Hoja zilizoibua mvutano ni upande wa muda wa Mwanasheria Mkuu wa serikali kujibu hoja zilizoibuliwa na waombaji uongezwe kama ilivyoombwa na upande wa AG au upunguzwe kama ilivyoombwa na upande wa waombaji.
Pia kama Mahakama iweke zuio (Injunction) la kuzuia muswada kujadiliwa Bungeni, kama ilivyoombwa na waombaji mpaka kesi ya msingi itaposikilizwa na kuamuliwa.
Leave a comment