Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Zimbabwe yatangaza mali za Mugabe
Habari Mchanganyiko

Zimbabwe yatangaza mali za Mugabe

Marehemu Robert Mugabe enzi za uhai wake
Spread the love

SERIKALI ya Zimbabwe imeanika mali zilizoachwa na aliyekuwa rais wa taifa hilo, Robert Mugabe, aliyefariki dunia Septemba 2019. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gazeti la Serikali ya Zimbabwe, The Herald, Mugabe ameacha Dola za Marekani Milioni 10 (Tsh. 22.9 bilioni), nyumba nne mjini Harare, magari 10, mashamba na bustani.

Hata hivyo, gazeti hilo halijaorodhesha mali za Mugabe zilizoko nje ya nchi, pamoja na biashara aliyokuwa anafanya na mke wake, Grace Mugabe.

Katika hali isiyo ya kawaida, inadaiwa kwamba Mugabe hajaacha wosia kuhusu wamiliki wa mali zake.

Terrence Hussein, aliyekuwa Mwanasheria wa Mugabe amesema yeye pamoja na familia ya Mugabe, hawajapata wosia ulioachwa na kiongozi huyo wa Zimbabwe.

Lakini, kwa mujibu wa sheria za Zimbabwe, mali ikiwemo mashamba ya mtu aliyefariki pasina kuacha wosia, hugawanywa kwa mke au mweza na watoto wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!