Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Zidane, Klopp, Flick vita tuzo ya kocha bora wa dunia
Michezo

Zidane, Klopp, Flick vita tuzo ya kocha bora wa dunia

Spread the love

MAKOCHA Zinedine Zidane wa Real Madrid, Jurgen Klopp wa Liverpool na Hans Flick anaekinoa kikosi cha Bayern Munich wameteuliwa kati ya makocha watano walioingia kwenye kinyang’anyiro cha tuzo ya kocha bora wa dunia kwa mwaka 2020 zinatolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA). Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Tuzo hizo ambazo hutolewa kila mwaka na shirikisho hilo ambazo zinatambulika kwa jina la Tuzo za FIFA (FIFA Awards) ambazo zitatolewa tarehe 17 Desemba, 2020 katika vipengele tofauti.

Kuingizwa kwa makocha hao ni kutokana na mafaniko makubwa waliyoyapata kwenye msimu uliopita huku Hans Flick akiongoza Bayern Munich kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) na Ligi Kuu nchini Ujerumani, mafanikio makubwa waliopata Klopp na Zidane ni kutwaa mataji ya Ligi Kuu nchini mwao.

Hans Flick

Katika orodha hiyo pia wamejumuishwa kocha wa Leeds United inayoshiriki Ligi Kuu England, Marcelo Bielsa, sambamba na kocha mkuu wa Sevilla ya Hispania, Julien Lopetegul.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!