Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Z’bar maambukizi ya corona yapanda
AfyaHabari Mchanganyiko

Z’bar maambukizi ya corona yapanda

Hamad Rashid Mohammed, Waziri wa Afya Zanzibar.
Spread the love

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza ongezeko la wagonjwa wapya sita wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa ya ongezeko hilo imetolewa leo tarehe 15 Aprili 2020, na Hamad Rashid Mohammed, Waziri wa Afya Zanzibar.

Taarifa ya Mohammed inaeleza kuwa, kufuatia ongezeko hilo, kwa sasa Zanzibar ina jumla ya wagonjwa 18 kutoka idadi ya watu 12 iliyokuwepo awali.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wagonjwa watano ni raia wa Tanzania ambao hawana historia ya kusafiri nje ya nchi siku za hivi karibuni, na mmoja ni raia wa Misri, aliyeingia nchini akitokea kwao kupitia Dubai kwa Shirika la Ndege la Fly Dubai.

Mohammed amesema wagonjwa wote wamelazwa katika vituo maalumu kwa ajili ya kuendelea na matibabu.

“Serikali kupitia wizara ya afya inaendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari zote za kujikinga na ugonjwa huu zinazotolewa mara kwa mara ikiwemo unawaji mikono kwa maji yanayotiririka na sabuyni , kuepuka misongamano na kuahirisha safari za nje na ndani ya nchi zisizo za lazima,” inaeleza taarifa ya Mohammed.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!