Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ZANU PF yamshinikiza Mugabe ajiuzulu
KimataifaTangulizi

ZANU PF yamshinikiza Mugabe ajiuzulu

Robert Mugabe, Rais wa Zimbabwe
Spread the love

CHAMA tawala Zimbabwe ZANU PF kimemtaka Rais Robert Mugabe ajiuzulu, kauli hiyo imetolewa na viongozi wa matawi ya chama hicho katika majimbo yote 10 yaliyokutana jana na yamemtaka Mugabe na mke wake Grace wajiuzulu.

Viongozi wa chama hicho wamesema watamshinikiza kiongozi huyo ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1980 kuondolewa kutoka uongozi wa chama hicho ifikapo hapo kesho Jumapili na baada ya hilo, bunge litapiga kura ya kutokuwa na imani naye.

Chama cha ZANU PF kitafanya mkutano maalamu wa kamati kuu siku ya Jumapili kujadili yanayojiri kisiasa nchini humo.

Mugabe alionekana kwa mara ya kwanza hadharani, katika mahafali ya chuo kikuu mjini Harare siku ya jana tangu jeshi lilipomuweka chini ya kifungo cha nyumbani wiki hii. Mkewe Grace hajaonekana hadharani tangu jeshi lilipochukua madaraka.

Jeshi la Zimbabwe linapata ugumu wa kuonyesha heshima kwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kwa kumuita rais na kamanda mkuu wa jeshi.

Taarifa kutoka kwa jeshi hilo imesema kuwa viongozi wake wanashauriana na Kamanda Mkuu wa jeshi Rais Robert Mugabe kuhusu njia bora ya kusonga mbele na litalifahamisha taifa baadaye kuhusu matokeo hayo haraka iwezekanavyo.

Kituo cha televisheni cha serikali ZBC kimeripoti kuhusu kuendelea kwa shinikizo kutoka kwa wanachama wa ZANU PF kwa Mugabe kujiuzulu. ZBC imekuwa ikitumika na serikali ya Mugabe kwa miongo kadhaa kueneza propaganda.

ZANU PF pia imeitisha maandamano leo katika mji mkuu, Harare kuliunga mkono jeshi kwa kuchukua madaraka na kumshinikiza Mugabe ajiuzulu.

Wananchi wa Zimbabwe wakiandama katika jiji la Harare wakishinikiza Rais Robert Mugabe ajihudhuru

Pia chama hicho kinataka makamu wa Rais aliyefutwa kazi Emmerson Mnangagwa arejeshwe katika wadhifa huo kwa sababu alifutwa kazi bila ya ridhaa ya kamati kuu ya chama hicho.

Wazimbabwe wengi wanahisi mipango ya jeshi ni kumkabidhi Mnangagwa madaraka. Huenda viongozi wa kijeshi wanasubiri Mnangagwa ambaye anajulikana kwa jina maarufu kama mamba arejeshwe katika wadhifa wa makamu wa rais kabla ya kumshinikiza Mugabe kuondoka madarakani kwa njia ya amani.

Mugabe anaheshimika sana kama kiongozi aliyepigania uhuru lakini pia wengi wanamuona kama Rais aliyeivuruga nchi yake kwa kusalia madarakani kwa muda mrefu.

Uchumi wa nchi hiyo umeporomoka vibaya, visa vya ufisadi, usimamizi mbaya, azma ya mke wake Grace kutaka kurithi madaraka na umri wake kuwa mkubwa ni mambo yanayowafanya Wazimbabwe kuhisi hana uwezo tena wa kuliongoza taifa hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Kimataifa

Tanzania, Italia kuimarisha ushirikiano sekta za kimkakati

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania na Italia zimeahidi kuimarisha ushirikiano katika...

Habari za SiasaTangulizi

CDF Mabeyo: Magufuli alijua anakufa

Spread the love  ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi nchini (CDF), Jenerali Venance Mabeyo,...

AfyaTangulizi

Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF

Spread the loveSERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa...

error: Content is protected !!