Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Yondani avuliwa unahodha Yanga, Ajibu achukua nafasi
Michezo

Yondani avuliwa unahodha Yanga, Ajibu achukua nafasi

Spread the love

KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amemvua unahodha, Kelvin Yondani kutokana na mchezaji huyo kutofika mazoezini bila taarifa yoyote, nafasi yake kuchukuliwa na  Ibrahim Ajibu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, imeeleza kikosi cha wachezaji wasioenda kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi kuendelea na mazoezi pamoja na kuondolewa kwa Yondani katika nafasi hiyo.

“Wachezaji waliobaki Dar es Salaam, wanaendelea na mazoezi leo katika viwanja vya polisi ufundi kurasini jijini Dar es Salaam baada ya mapumziko ya siku nne kwa baadhi ya wachezaji ambao hawakusafiri na timu visiwani Zanzibar kwenye michuano ya kombe la Mapinduzi.” Ilienda sehemu ya taarifa hiyo.

Siyo mara ya kwanza kocha huyo kuchukua maamuzi magumu kwa baadhi ya wachezaji ndani ya kikosi hicho kutokana kuhitaji usawa na nidhamu kwa wachezaji wote ndani ya klabu hiyo kiasi cha hivi karibuni kumuondoa katika kikosi kipa namba moja wa timu hiyo, Beno Kakolanya baada ya kuondoka kambini bila taarifa kwa kushinikiza alipwe madai yake.

Mazoezi hayo yaliongozwa na kocha huyo yalikuwa ya utimamu wa mwili pia kwa upande wa uwanjani kulikuwa na mafunzo maalumu juu ya umakni uwanjani (Concentration) pamoja na umaliziaji kwenye safu ya ushambuliaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!