KLABU ya Yanga imewaomba radhi kiungo wa JKT Tanzania, Mwinyi Kazimoto na tiju yake, huku ikimwadhibu beki wake, Lamine Moro raia wa Ghana, kwa kitendo cha utovu wa nidhamu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Lamine ameadhibiwa kwa kukatwa Tsh. 1,000,000 kwenye mshahara wake mara baada ya kuonesha kitendo kisicho cha uungwana kwa kumpiga teke Kazimoto.
Kitendo hicho kilichomfanya beki huyo kutolewa nje na mwamuzi Lodivic Charles kutoka Mwanza, kwa kumuoneshea kadi nyekundu katika dakika 89 ya mchezo.
Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo iliyotoka muda mfupi mara baada ya mchezo huo kukamalika imeeleza kuwa, licha ya mchezaji huyo kuomba radhi lakini uongozi umeamua kumchukulia hatua kwa mujibu wa kanuni na taratibu za klabu.
Lakini pia Yanga imeomba radhi kwa wapenzi wa mpira wa miguu nchini sambamba na kiungo wa klabu ya Jkt Mwinyi Kazimoto.
Lamine Moro ataoukosa mchezo ujao dhidi ya Azam FC utakaofanyika siku ya Kumapili, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Leave a comment