Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga sasa kuja kidigitali
Michezo

Yanga sasa kuja kidigitali

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten (kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Charles Mkwasa
Spread the love

KLABU Yanga imezindua kipindi cha televisheni kilichopewa jina la ‘Yanga TV Show’ sambamba na mfumo wa kuwapa habari wanachama wake utakaoitwa ‘Yanga Kidigitali’ vinavyotarajiwa kuanza Aprili Mosi Mwaka huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kipindi cha Yanga TV Show kitakuwa kinarushwa kupitia kituo cha televisheni cha Azam TV wakati mfumo wa kutoa habari kwa wanachama wa Yanga Kidigitali utakuwa unapitia kampuni ya simu za mkononi za Tigo pamoja ya Prime.

Meneja wa michezo wa Azam Tv, Baruhan Muhuza amesema wameingia makubaliano na klabu ya Yanga ya uanzishwaji wa kipindi hicho baada ya majadiliano ya muda mrefu ili kufanya kipindi hicho kuwa cha tofauti.

“Yanga TV Show itakuja na muonekana mpya na wakipekee kwa kuwa itahusisha wachezaji wa zamani wa klabu hii kufanya uchambuzi katika michezo iliopita na itakayokuja katika Ligi Kuu pamoja na kuwajua mwenendo mzima wa timu inapokuwa ndani na nje ya Uwanja,” amesema Muhuza.

Aidha aliongezea ya kuwa Yanga kuwa na kipindi cha televisheni itakuwa fulsa kwa klabu katika kujiongezea mapato kwa kuwa kipindi kinaweza kupata wadhamini kutokana na kuwa cha tofauti na kufanya klabu hiyo iweze kujiendesha yenyewe kwa kuwa na vyanzo vingi vya mapato.

Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa amesema kuanzisha Yanga TV Show na Yanga Kidigitali ni mikakati ya kuwapa fulsa wanachama wa klabu hiyo kupata habari za timu yao ikiwa pamoja na kujipatia kipacho ambacho kitaifanya waweze kujitegemea kwa kipato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!