Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga mguu sawa kuikabili Kagera
Michezo

Yanga mguu sawa kuikabili Kagera

Spread the love

USHINDI wa mabao 3-2 dhidi ya Ndanda FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kikosi cha Yanga kimejiimalisha kuikabili Kagera Sugar, katika mchezo wa kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga wanatarajia kuikabili Kagera Sugar,  tarehe 30 Juni, 2020 kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika harakati ya kutafuta tiketi ya kufuzu nusu fainali ya kombe hilo.

Mabao ya Yanga kwenye mchezo wa leo yamefungwa na Deusi Kaseke (6, 45+2) na baadae kufuatia na bao la ushindi la Mrisho Ngassa (73) aliyeingia kuchukua nafasi ya Ditram Nchimbi.

Kwa upande wa Ndanda FC,  mabao yao yalipachikwa na Abdul Hamis (10) na dakika tano baadae Vitaris Mayanga akaandika bao la Pili kwa mpira wa adhabu ndogo.

Kwa matokeo hayo Yanga inajisogeza mpaka nafasi ya pili baada ya kufikisha pointi 59, ikiwa tofauti ya pointi moja na Azam Fc ambao wamelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Biashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!