ALIYEKUWA nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ”Cannavaro” anatarajiwa kuagwa rasmi ndani ya klabu hiyo tarehe 12 Agosti, 2018 kwa mchezo maalumu wa kirafiki baada ya kutangaza kutundika daruga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Katika taarifa rasmi iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo kupitia kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii, imesema klabu hiyo inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki na timu ambayo bado haijafaamika kwa lengo la kumuaga nahodha huyo.
Cannavaro ambaye alitangaza kustaafu soka 26 Juni, mwaka huu, amefanikiwa kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka 12, toka alipojiunga nayo Mwaka 2006 akitokea Malindi FC, inayoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.
Yanga ambayo kwa sasa imeweka kambi mkoani Morogoro kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu pamoja na mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger unaotarajia kuchezwa 19 Agosti, 2018.
Leave a comment