Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12
Michezo

Yanga kumuaga rasmi Canavaro Agosti 12

Spread the love

ALIYEKUWA nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ”Cannavaro” anatarajiwa kuagwa rasmi ndani ya klabu hiyo tarehe 12 Agosti, 2018 kwa mchezo maalumu wa kirafiki baada ya kutangaza kutundika daruga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo kupitia kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii, imesema klabu hiyo inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki na timu ambayo bado haijafaamika kwa lengo la kumuaga nahodha huyo.

Cannavaro ambaye alitangaza kustaafu soka 26 Juni, mwaka huu, amefanikiwa kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka 12, toka alipojiunga nayo Mwaka 2006 akitokea Malindi FC, inayoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.

Yanga ambayo kwa sasa imeweka kambi mkoani Morogoro kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu pamoja na mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger unaotarajia kuchezwa 19 Agosti, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!