Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kujipima ubavu kwa Mlandege
Michezo

Yanga kujipima ubavu kwa Mlandege

Spread the love

TIMU Yanga kesho itacheza mchezo wa kujipima nguvu dhidi mabingwa wa Ligi Kuu visiwani Zanzibar, Mlandege katika kujiweka sawa kuwakabili Kagera Sugar kwenye mchezo ujao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga itacheza mchezo huo majira ya Saa 1 jioni kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamanzi kabla ya kusafiri kwenda mkoani Kagera kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa siku ya Jumamosi 18 septemba, 2020 kwenye dimba la Kaitaba.

Mchezo huo ambao utakuwa na umuhimu mkubwa kwa Yanga ili kujiweka sawa kwa kuwa imefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi chake ambacho kina wachezaji wapya zaidi ya 12.

Yanga inaingia kwenye mchezo huo, huku ikiwa imeshacheza michezo miwili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na kuambulia alama 4, baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City na kutoka sare na Tanzania Prisons.

Mlandege FC wao watatumia mchezo huo kujiweka sawa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi na michuano ya kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!