KINDA wa klabu ya Liverpool, Ben Woodburn (17), ameweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga goli akiwa na umri mdogo katika historia ya klabu hiyo toka kuanzishwa kwake, anaandika Kelvin Mwaipungu.
Woodburn ameweka rekodi hiyo akiwa na umri wa miaka 17 na siku 45 baada ya kufunga goli katika mchezo ambao Liverpool waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Leeds United kwenye hatua ya robo fainali ya Kombe la Ligi.
Awali rekodi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo Michael Owen aliyeiweka mwaka 1997 dhidi ya Wimbledon akiwa na umri wa miaka 17 na siku 98 na rekodi hiyo ilidumu kwa miaka 13.
Another record taken from me!!! Congratulations @BenWoodburn on becoming the youngest ever scorer for @LFC at 17yrs and 45days. #KopEnd
— michael owen (@themichaelowen) November 29, 2016
Baada ya Woodburn kuweka rekodi hiyo jana usiku, Owen alimpongeza mchezaji huyo kupitia ukurasa wake wa kwenye mtandao wa Twitter saa chache baada ya mchezo kumalizika kwa kuweka rekodi hiyo.
A lot of players who came through the academy & had big careers make an impact early through goals, Fowler, Owen, Woodburn & Carragher! ⚽️
— Jamie Carragher (@Carra23) November 29, 2016