Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wilaya 27 hazina mahakama za wilaya-Dk. Mahiga
Habari Mchanganyiko

Wilaya 27 hazina mahakama za wilaya-Dk. Mahiga

Spread the love

SERIKALI imesema, ni kweli Wilaya ya Itilima kwa sasa haina Mahakama ya Wilaya, hivyo wananchi wanalazimika kusafiri kwa umbali wa kilometa 37 kufuata huduma katika Wilaya ya Bariadi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Hayo yameelezwa leo tarehe 11 Agosti 2019 bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Gimbi Masaba (Chadema).

Katika swali na msingi la mbunge huyo, alitaka kujua ni lini serikali itajenga mahakama ya wilaya katika Wilaya ya Itilima?

Dk. Mahiga akijibu swali la msingi amesema, ni kweli wilaya hiyo haina Mahakama ya Wilaya na wananchi wanalazimika kusafiri kwa umbali wa kilometa 37 kufuata huduma katika wilaya ya Bariadi.

Aidha, amesema kuwa changamoto hiyo ipo katika wilaya 27 nchini ambazo zinapata huduma katika wilaya za jirani, na hali hiyo inatokana na ukweli kwamba Mahakama ya Tanzania bado inakabiliwa na uhaba wa majengo katika maeneo mengi.

“Kama ambavyo nimekuwa nikieleza katika bunge lako tukufu, mahakama imejiwekea mkakati wa kutatua changamoto hii, hatua kwa hatua kupitia mpango wake na miaka mitano ya kujenga na kukarabati majengo ya mahakama kwa ngazi zote.

“Mahakama ya Wilaya ya Itilima ipo katika mpango wa kujengwa katika mwaka wa fedha 2019/20 pamoja na mahakama nyingine katia wilaya ya Busega, Kyerwa, Misenyi, Gairo, Mbogwe, Songwe,Nyang’wale,Mvomero pamoja na wilaya nyingine zenye uhitaji” ameeleza Dk. Mahiga.

Aidha amesema, anashukuru uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Itilima kwa kutoa kiwanja cha kujenga mahakama ya wilaya, chenye ukubwa za mita za mraba 5,028.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!