Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wezi wapora vifaa vya NIDA, wawili wanaswa
Habari MchanganyikoTangulizi

Wezi wapora vifaa vya NIDA, wawili wanaswa

Spread the love

WATU wasiojulikana wametoweka na vifaa vya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), wilayani Arumeru, Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Watu hao wameiba kompyuta mpakato (laptop) mbili, kompyuta (Desk top) moja, stendi mbili, kamera mbili, stendi mbili, Extation mbili na keyboad moja.

Kwa mujibu wa Jerry Muro, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, vifaa hivyo vimeibwa usiku wa kuamkia leo tarehe 6 Januari 2020, katika ofisi hizo zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.

Muro amesema, kinachofanywa kwenye wilaya hiyo ni hujuma, kwa kuwa, si mara ya kwanza kwa ofisi za NIDA kuvamiwa na kuporwa vitu hivyo.

“Hii si mara ya kwanza wizi wa namna hii kutokea, ule wa awali mpaka sasa upelelezi wake bado unaendelea,” amesema Muro na akiongeza “hii nihujuma inayofanywa kwenye wilaya hii.”

Kutokana na mkasa huo, watu wawili mpaka sasa wanashikiliwa wakihusishwa na wizi huo. Wanaoshikiliwa ni Asheri Lorubani ambaye ni mlinzi na Wilson Laizer, muhudumu wa ofisi hiyo.

Licha ya Muro kuagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini waliohusika, pia amewaomba wananchi kutoa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!