Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Wema Sepetu azidi kusota mahakamani
Michezo

Wema Sepetu azidi kusota mahakamani

Wema Sepetu (kulia) akitoka na mama yake mahakamani Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imehailisha usikilizwaji wa kesi  ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili msanii wa Filamu nchini Wema Sepetu mpaka Novemba 24, mwaka huu, anaandika Faki Sosi.

Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba ambapo leo upande wa Jamhuri ulidai kuwa utafika mahakamani hapo na mashahidi wawili.

Wema  alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Februari 22, mwaka huu pamoja na Matilda Abass na Angelina Msigwa waliotajwa kuwa ni wafanyakazi wake wa ndani na kusomewa shitaka moja la utumiaji dawa ya kulevya aina ya bangi. Alikana shitaka.

Awali Oktoba 31, mwaka huu, mahakama hiyo ilitoa uamuzi wa mapingamizi yaliyowasilishwa na wakili wa utetezi Peter Kibatala wa kupinga hati ya ukamataji mali iliyowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka.

Hakimu Simba alipokea hati hiyo ya baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili na kuingiza kwenye rekodi za mahakama hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!