Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji
Habari Mchanganyiko

Wazungu wadaiwa kumteka kimafia MO Dewji

Mohamed Dewji 'MO Dewji'
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limeeleza kuwa, linawashilikia watu watatu wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kutekwa kwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji, lililotokea alfajiri ya leo tarehe 11 Oktoba 2018, katika Gym ya hoteli ya Colosseum iliyoko Oysterbay jijini Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewaambia wanahabari kuwa, MO Dewji anayedaiwa kutekwa kimafia, alitekwa na wazungu wawili waliokuwa na silaha za moto.

Kamanda Mambosasa ameeleza kuwa, wazungu hao wawili waliwasilia hotelini hapo wakiwa na gari binafsi aina ya Surf ambalo walilipaki karibu na gari ya MO Dewji, kisha kumchomo mfanyabiashara huyo ndani ya gari lake na kumpakia kwenye gari lao, na kuondoka naye kusikojulikana.

Kwa mujibu wa taarifa za awali zilizo tolewa na mashuhuda wa tukio hilo, inasemekana watu hao walikuwa wanne huku wakiwa wamefunika nyuso zao ‘Ninja’, walifyatua risasi hewani kuwatishia watu waliokuwa karibu na eneo hilo kabla ya kuondoka naye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!