WAZIRI wa Usafirishaji wa Zimbabwe, Joel Biggie Matiza, amefariki dunia jana Ijumaa tarehe 22 Januari 2021, katika Hospitali ya St. Anne Harare nchini humo, alipokuwa anatibiwa maambukizo ya virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Matiza anakuwa waziri watatu wa Zimbambwe kufikwa na mauti kwa corona ndani ya wiki moja iliyopita.
Tarehe 20 Januari 2021, Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara, Dk. Sibusiso Moyo (58), alifariki dunia katika moja ya hospitali nchini humo alipokuwa akitibiwa maambukizo ya corona.
Waziri mwingine aliyefariki kwa corona ndani ya wiki moja ni Ellen Gwaradzimba ambaye ni waziri wa nchi, anayeshughulikia masuala ya mikoa aliyefariki tarehe 15 Januari 2021.
Pia, Morton Malianga (90), aliyewahi kuwa naibu waziri wa fedha, alifariki dunia tarehe 15 Januari 2021.
Leave a comment