WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Phillip Mpango ametakiwa kutoa idadi ya wananchi waliotolewa kwenye unyonge wa umasikini, tangu serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akichangia hoja leo tarehe 7 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amehoji kuwa, tangu serikali ya Rais John Magufuli ilipoingia madarakani ilikuta idadi ya wanyonge wangapi na walioondolowe kwenye unyonge huo ni wangapi.
Katika hatua nyingine, Heche amehoji mahali zilipo fedha zilizokusanywa na serikali ikiwa baadhi ya wananchi wanalia fedha hazionekani mitaan, i huku serikali ikijinasibu kwamba inakusanya fedha nyingi.
Wakati akichangia hoja kuhusu mapendekezo ya mpango wa taifa wa maendeleo wa mwaka 2019/20, Heche ameeleza kwamba, serikali imeshindwa kutekeleza mpango wake wa kupelekea fedha za maendeleo kwa mwaka wa fedha wa 2017/18 ambapo ilipeleka Sh.6 trilioni badala ya Sh. 12 trilioni ilizopanga kupeleka.
Leave a comment