Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri wa Fedha Kenya ajisalimisha
Kimataifa

Waziri wa Fedha Kenya ajisalimisha

Henry Rotich, Waziri wa Fedha wa Kenya
Spread the love

HENRY Rotich, Waziri wa Fedha nchini Kenya amejisalimisha kwa maafisa wa upelelezi, saa kadhaa baada ya Noordin Haji, Mkurugenzi wa Mashtaka kuagiza akamatwe. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Rotich amejisalimisha katika makao makuu ya Idara ya Upelelezi nchini Kenya leo tarehe 22 Julai 2019, kuitikia wito wa Haji.

Ni kuhusu tuhuma zinazomkabili za kukiuka muongozo wa utoaji wa kandarasi ya ujenzi wa mabwawa, wenye thamani zaidi ya Dola za Marekani 450 milioni, iliyopewa Kampuni ya Italia ya CMC de Ravenna.

Kwa mujibu wa mitandao ya Kimataifa, Rotich anahojiwa na maafisa wa upelelezi, baada ya Haji kueleza kwamba waziri huyo wa fedha pamoja na baadhi ya viongozi wengine waandamizi nchini Kenya watashtakiwa kwa kupanga udanganyifu kutokana na kushindwa kutii muongozo unaotumika katika upatikanaji wa kandarasi.

Tuhuma hizo dhidi ya Rotich ziliibuka mwanzoni mwa mwaka huu, ambapo mwezi Machi waziri huyo alikana tuhuma hizo. Vile vile, kampnuni ya Italia CMC de Ravenna ilikana kuhusika katika tuhuma hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!