Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Nchemba aridhia wakimbizi kurudi kwao
Habari Mchanganyiko

Waziri Nchemba aridhia wakimbizi kurudi kwao

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema serikali ya Tanzania haifukuzi wakimbizi kama inavyodaiwa, anaandika Hamisi Mguta.

Mwigulu amesema hayo katika kikao cha kuweka maandalizi ya kuwarejesha wakimbizi raia wa Burundi ambao walioomba kwa ridhaa yao kurudi nchini kwao.

“Serikali ya Tanzania haifukuzi wakimbizi, tunaunga mkono hiari yao ya kuondoka, wenyewe kwa kuwa waliishinikiza serikali kwa kufanya fujo ili walirudishwe kwao na mimi kama waziri mwenye dhamana niliwaambia sitaongeza polisi kupambana na watu wanaotaka kurudi kwao,” amesema.

Amesema kuwa Tanzania inaendelea na majukumu yake yaliyobainishwa kwenye mikataba ya kimataifa ya kupokea na kutunza wakimbizi na mpaka sasa Tanzania ina Wakimbizi zaidi ya 351,400 kutoka Burundi na Kongo.

“Wakimbizi 73,000 wanatoka Kongo na 277,535 wanatoka Burundi. na 150 ni wabantu kutoka Somalia na 338 ni wa kutoka mataifa mengine,”amesema.

Aidha, ameeleza kuwa sheria za kimataifa zinaelekeza kwamba kama watu watajiandikisha kwa ridhaa yao kwamba wanataka kurudi walipotoka na wana uhakika kuwa sababu iliyowafanya wakimbie haipo tena.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!