Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri mwingine awekwa rehani bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Waziri mwingine awekwa rehani bungeni

Spread the love

MBUNGE wa Monduli (CHADEMA), Julius Karanga, ametuhumu serikali kuwanyonya wafugaji nchini na kusema, “wakati wengine (Chama Cha Mapinduzi), wakifikiri mifugo ni chakula, wao (Chadema), wanaiona mifugo kuwa ni uchumi.” Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni wakati wa kuchangia mjadala wa bajeti ya wizara ya Uvuvi na Mifugo bungeni leo Alhamisi, Kalanga alisema, kwa miaka mitatu mfululizo sasa, serikali haijaweza kupeleka kwenye wizara hii, hata shilingi ya fedha maendeleo.

Alisema, “ndani ya kipindi cha miaka mitatu, serikali haijapeleka hata shilingi kwenye miradi ya maendeleo kupitia wizara hii. Ndani ya miaka mitatu, hakuna miradi yoyote ya maendeleo iliyotekelezwa kwenye wizara ya uvuvi na mifugo.”

Akaongeza: “Kinachoonekana kwenye bajeti, ni mbio za serikali za kutokomeza wafugaji, kuuwa viwanda vya ndani na kutumia mabilioni ya shilingi kuagiza bidhaa za nyama na samaki nje ya nchi.”

Kwa mujibu wa Kalanga, serikali inapoteza kiasi cha Sh. 120 bilioni kila mwaka kwa kuagiza maziwa; Sh.34 bilioni kwenye ngozi na huagiza takribani tani 4000 (elfu nne) za nyama kila mwaka.

Mapema waziri wa wizara hiyo, Luhaga Mpina aliliambia Bunge kuwa wizara yake imejipanga kutatua matatizo ya wafugaji na kuzipatia ufumbuzi changamoto za kilimo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!