Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Mpango kugombea jimbo la Mbunge wa CCM
Habari za Siasa

Waziri Mpango kugombea jimbo la Mbunge wa CCM

Dk. Philip Mpango
Spread the love

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango ametangaza ‘kiaina’ kuwania Ubunge wa Buhigwe mkoani Kigoma kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Albert Obama kupitia CCM. Obama amewaongoza wananchi wa Buhigwe tangu mwkaa 2010.

Dk. Mpango alitangaza adhima hiyo jana Alhamisi tarehe 11 Juni 2020 Bungeni jijini Dodoma, wakati akihitimisha hotuba ya Bajeti ya Serikali ya Tanzania ya mwaka 2020/21 ya Sh. 34.87 trilioni.

Katika hitimisho lake, Dk. Mpango alitoa pongezi lukuki kwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli jinsi alivyoliongoza Taifa hilo kwa kipindi cha miaka mine na ushehe na kuwaomba Watanzania kumchagua tena kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Mbunge wa Buhigwe, Albert Obama

Dk. Mpango ambaye ni Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, alitumia fursa hiyohiyo kutangaza nia akisema, “Watanzania msisahau pia kumpatia Rais wetu wabunge na madiwani wanaomudu maadili na mwendo wa Hapa kazi Tu na kama itawapendeza wananchi wenzangu wa Buhigwe na chama chetu (CCM), basi iwe pamoja na mimi mtumishi wenu.”

Baada ya kueleza hivyo, ukumbi karibia wote wa Bunge, ulilipuka kwa shangwe za kushangilia kwa makofi na vigelegele.

Akiendelea kuhitimisha, Dk. Mpango alisema, “Nawaambia kweli Watanzania wenzangu, Rais huyu ni tunu ya thamani kubwa kwa Tanzania na utawala wake ni fursa kubwa ambayo kama hatutaitumia vizuri, basi mjue itachukua miaka mingi ijayo kuifikia Tanzania mpya tunayoitamani.

1 Comment

  • CCM internal rifts will be beneficial to the opposition camp especially Chadema!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!