Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Masauni kada wa 17 kuchukua fomu CCM Z’bar
Habari za Siasa

Waziri Masauni kada wa 17 kuchukua fomu CCM Z’bar

Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania akichukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM
Spread the love

HAMAD Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi leo tarehe 22 Juni 2020, amejitokeza kuchukua fomu kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar kugombea urais. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kada huyo na waziri alijitokeza katika ofisi kuu za CCM zilizopo Kisiwandui mjini Zanzibar.

Masauni anafanya idadi ya makada wa chama hicho waliojitokeza kuomba kuteuliwa visiwani humo kufika 17. Miongoni mwa waliojitokeza mpaka sasa ni Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar; Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Ulinzi.

Wengine ni Balozi Ali Karume, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Sheikh Abeid Aman Karume: Jecha Salim Jecha, aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi na Omar Sheha Mussa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!