Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki
Habari za Siasa

Waziri Kairuki akumbuka vyeti feki

Angela Kairuki, Waziri wa Madini
Spread the love

ALIYEKUWA  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki leo ameaga  ofisi yake ya zamani huku akikumbuka alivyohangaika na watumishi waliokuwa na vyeti feki. anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kairuki amesema katika kipindi cha miezi 23 tangu ateuliwa kuongoza wizara hiyo, amekumbana na changomoto nyingi.

Amesema suala la vyeti feki ambalo liliwakumba watumishi wa serikali wapatao 12,000 ulikuwa ni mtihani mkubwa kwake wakati akiongoza wizara hiyo ambayo ipo chini ya Rais.

“Baadhi ya maofisa utumishi hawakuwa waaminifu walikuwa wanawaficha wale wenye feki,  lakini suala hilo tulilikamilisha kwa kiasi kikubwa,’’ amesema

Kwa upande wake, Waziri mpya wa wizara hiyo, George  Mkuchika ameahidi kuendeleza kasi na nidhamu kwa watumishi wa umma.

Kairuki ameteuliwa kuwa Waziri wa Madini kumrithi mtangulizi wake, George Simbachawene ambaye alitimuliwa kazi kutokana na kutajwa katika ripoti ya Bunge iliyochunguza madini ya Almasi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!