Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Kabudi apata ajali
Habari za Siasa

Waziri Kabudi apata ajali

Prof. Palamagamba Kabudi
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amepata ajali ya gari mkoani Morogoro leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Akizungumza nje ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro, Mkuu wa Mkoa huo, Loata Sanare amesema, leo walikuwa na ziara wilayani Kilosa na tayari walikwisha kufika lakini baadaye walipata taarifa  Waziri Kabudi amepata ajali.

Kabudi naye alikuwa anakwenda Kilosa ambako yeye ni mbunge mteule wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Madaktari wamemcheki hana tatizo kubwa sana, anahitaji kupumzika. Niwatoe wasiwasi  wana Kilosa na Watanzania, Mzee Kabudi amepata ajali lakini anaendelea vizuri,” amesema.

Sanare amesema, baada ya mapumziko aliyopewa Waziri Kabudi, watapata maelekezo mengine ya nini cha kufanya.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!