Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wazee Ubungo walamba bingo  kutibiwa bure
Habari Mchanganyiko

Wazee Ubungo walamba bingo  kutibiwa bure

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya akitoa kitambulisho cha kupatiwa huduma ya afya bure katika halmashauri ya Ubungo
Spread the love

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amezitaka hosptali za wilaya kuanzisha dirisha  maalum la wazee ili kuwapunguzia changamoto pindi wanapohitaji huduma za matibabu, anaandika Hamisi Mguta.

Waziri Mwalimu ameyasema hayo jana katika Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa matibabu ya bure kwa wazee ambayo itatolewa kwa wazee waishio ndani ya eneo hilo ambao wanafikia 7,299.

Wazee  wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa malipo kwa huduma za afya katika hospitali za serikali.

“Kuwa na vitambulisho ni jambo moja na kupata huduma ni jambo la pili, vitambulisho hivi viwe sehemu ya wazee kupata huduma bora za afya, siyo mzee anaenda na kitambulisho anaambiwa dawa hakuna kanunue, hakutakuwa na ulazima kupatiwa vitambulisho,” amesema

Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, amaesema Sh.  1.805 kwa mwaka zitatumika kwa mwaka mmoja ili kuwahudumia  wazee hao kwa vipimo, matibabu na vifaa tiba bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!