Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wazazi, walezi wapewa neno
Afya

Wazazi, walezi wapewa neno

Neema Rusibamaiya, Mkurugenzi wa Huduma ya Chanjo wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia Wazee na Watoto
Spread the love

WAZAZI na walezi kuwatunza na kiwalea watoto wa chini ya miaka mitano ikiwamo kuwapatia lishe bora, elimu na kuwalinda dhidi ya unyanyasaji, anaandika Angela Willium.

Kauli hiyo imetolewa leo na Taasisi ya Maendeleo ya Binadamu Chuo Kikuu cha Aga Khani na kusisitiza kuwa hatua hiyo itawasaidia watoto hao kukua.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma ya Chanjo katika Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Neema Rusibamaiya amewataka wazazi wanatakiwa kuwapatiwa watoto lishe bora, kukaa nao pamoja, kucheza nao na kuwasemesha hata kama hawajaanza kuongea kwa kuwa hatua hiyo inasaidia kuwakuza kiakili.

‘’Familia inatakiwa kuwalinda watoto dhidi ya watu wanaowanyanyasa kwa kuwa wanasababisha maendeleo yao kurudi nyuma hivyo kama kuna unyanyasaji mzazi asikae kimya.’’

Aidha, mwakirishi wa taasisi ya Aga Khan, Leonard Chumo amesema wamewekeza katika masuala ya elimu, afya na lishe bora lengo likiwa ni kuangalia haki za watoto chini ya miaka 5.

Chumo amesema wadau kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uganda , Kenya na serikali wamekutana leo katika kujadili namna ya kuwasaidia watoto ili waweze kukua vizuri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!