Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wawili wafariki dunia ajalini Pwani
Habari Mchanganyiko

Wawili wafariki dunia ajalini Pwani

Spread the love

WATU wawili wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa, katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 4 Septemba mwaka huu, iliyohusisha magari mawili ambayo yamegongana uso kwa uso katika barabara ya Dar es Salaam -Morogoro eneo la Mbala, Chalinze Mkoani Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani,(ACP) Wankyo Nyigesa akisema kuwa imetokea usiku wa kuamkia leo majira ya saa 9.30 alfajiri.

Akielezea kuhusu tukio hilo, ACP Nyigesa amesema gari namba T.542 DMJ/ 680 DKS aina ya Howo mali ya kampuni ya Gulf Agent ikitoka Dar es salaam kuelekea Chalinze ikiendeshwa na dereva Ramadhani Kibingo ( 38) mkazi wa Mbagala iligongana na gari T.405 DLV/ 904 DMN aina ya Daf mali ya kampuni ya RAS Logistic (T) ltd iliyokuwa ikitokea Morogoro kuelekea Dsm ikiendeshwa na dereva ambaye jina lake bado halijafahamika.

Amesema waliofariki dunia ni dereva huyo wa gari yenye namba T.405 DLV/904 DMN aina ya Daf na tingo wake ambao bado majina yao hayajafahamika.

Wankyo aliwataja majeruhi kuwa ni dereva Ramadhani Kibingo na tingo wake Ibrahim Said, Mzigua (28), mkazi wa Dar es salaam waliokuwa ndani ya gari T.542DMJ/680 DKS.

Miili ya marehemu imepelekwa hospital ya rufaa Tumbi kwa uchunguzi na kuhifadhiwa na majeruhi wamepelekwa kituoa cha afya Chalinze kwa ajili ya matibabu na hali zao sio mbaya, wakati dereva wa gari T.542 DMS/680 DKS aina ya Howo ,anashikiliwa chini ya ulinzi wa polisi kituo cha afya Chalinze.

Chanzo cha ajali ni dereva huyo ambae anadaiwa alijaribu kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhali na kugongana uso kwa uso na gari T.504 DLV/904 DMN aina ya DAF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!