Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watumishi Chadema wahusishwa uchomaji ofisi yao Arusha
Habari Mchanganyiko

Watumishi Chadema wahusishwa uchomaji ofisi yao Arusha

Ofisi za Chadema Arusha
Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha nchini Tanzania, limewakamata watu watatu wakituhumiwa kuchoma moto ofisi za chama kikuu cha upinzani nchini humo Chadema, Kanda ya Kaskazini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Ofisi hizo zilichomwa moto usiku wa kuamkia tarehe 14 Agosti 2020 na watu wasiojulikana na kusababisha uharibifu wa mali.

Leo Alhamisi tarehe 3 Septemba 2020, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Salum Hamduni ametoa taarifa kwa umma kuhusu tukio hilo akisema linawashikilia watu watatu ambao watapandishwa kizimbani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kamanda Hamduni amewataka watuhumiwa hao ni, Deogratius Malya, aliyekuwa mlinzi wa ofisi hiyo, Leonard Nkukula, dereva wa Chadema na Proster Makonya ambaye ni afisa mhamasishaji wa chama hicho makao makuu.

“Baada ya kukamilika kwa upelelezi, jalada la kesi hii limepelekwa ofisi ya taifa ya mashtaka kwa ajili ya kulisoma na kulitolea maamuzi au maelekezo ya kisheria ikiwa ni pamoja na kuandaa hati ya mashtaka,” amesema Kamanda Hamduni.

“Watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili baada ya kukamilika kwa taratibu za kisheria,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!