Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watuhumiwa wa mauaji ya Dk. Mvungi waachiwa, wakamatwa
Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya Dk. Mvungi waachiwa, wakamatwa

Spread the love

WATUHUMIWA wa maauji ya Dk. Sengodo Mvungi aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wameachiwa huru na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada Serikali kuomba kuondolewa kwa shitaka hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Watuhumiwa hao sita wameachiwa huru leo baada ya mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuomba kuondolewa kwa shitaka hilo na kwamba hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Watuhumiwa hao ni pamoja na Msigwa Matonya, Mianda Mlewa, Paulo Mdonondo, Longishu Losindo, Juma Kangungu na John Mayunga.

Wakili mkuu wa serikali Nasoro Katuga, aliwasilisha maombi hayo na mahakama ikakubali kuwaachia washtakiwa hao huru.

Baada ya kuachiwa huru walikamatwa tena na kupelekwa Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka mapya ya mauji ya Dk. Mvungi.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo la mauaji ya kukusudia siku ya jumapili terehe 3 Novemba mwaka 2013, eneo Msakuzi Mbezi jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!