Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano
KimataifaTangulizi

‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano

Mfano wa mtu aliyefanya mashambulizi katika Chumba cha habari cha gazeti la Capital Gazette la Marekani. Picha ndogo ofisi za gazeti hilo
Spread the love

WATU wasiojulikana wamevamia ofisi za gazeti la Capital Gazette na kufyatua risasi na kuua watu watano na kuwajeruhi wengine, katika jiji la Maryland, Marekani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mmoja wa wafanyakazi wa gazeti hilo amesema kuwa mtu aliyefyatua risasi katika chumba cha habari kupitia kwenye dirisha la vioo.

“Tukiwa kwenye madawati yetu katika chumba cha habari, tulistuka kusikia mtu akikoki bunduki na ghafla kuanza kusikia milio la risasi. Ni tukio la kustiha sana sana.” Aliandika mmoja ya waandishi walionusurika, Phil Davis katika ukurasa wake wa Twitter.

Polisi wameimarisha ulinzi katika eneo hilo na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

“Hili ni tukio baya sana lililotokea mchana huu,” alisema Mtendaji wa eneo hilo, Steve Schuh katika mkutano na waandishi wa habari. “Watu kadhaa wamefariki katika tukio hilo.”

Polisi wamesema kwa sasa hawawezi kutambua hasa ni aina gani ya silaha iliyotumika, lakini uchunguzi unaendelea wakisaidia na FBI na taasisi nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!