WATU takribani 188 wanahofiwa kupoteza maisha kwenye ajali ya ndege ya abiria ya Shirika la Lion Air iliyokuwa safarini kutoka mji mkuu wa Indonesia, Jarkata kuelekea mji wa Pangkal Pinang. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Ndege hiyo yenye safari namba JT-610 iliyoondoka mjini Jakarta siku ya Jumatatu majira ya saa 06:20 (23:30 GMT Jumapili kwa saa za Afrika Mashariki) imeangukia baharini Baada ya kusafiri kwa muda mfupi.
Ndege hiyo aina ya Boeing 737 namba JT-610 kabla ya kuangukia baharini ilipoteza mitambo ya rada baada ya kupaa ilipokuwa inavuka bahari.
Msemaji wa Shirika la Huduma za Uokoaji na utafutaji wa manusura, Yusuf Latif amethibitisha kuhusu tukio hilo, na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Naye Afisa wa Bandari nchini humo, Tanjung Priok amesema shughuli za uokoaji manusura zimeanza ambapo vyombo vya bahari ikiwemo boti na meli zimebeba waokoaji kuelekea eneo la tukio.
Leave a comment