Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watu 1,000 waugua Dengue Dar
Afya

Watu 1,000 waugua Dengue Dar

Mbu wanaambukiza ugonjwa wa Dengue
Spread the love

WATU takribani 1,000 wameugua ugonjwa wa Dengue Jijini Dar es Salaam kuanzia mwezi Januari hadi mwezi Mei 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hayo amesema Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk. Yudas  Ndungile leo tarehe 11 Mei 2019 wakati akizungumza na kituo moja cha redio  hapa nchini.

Dk. Ndungile amesema ugonjwa wa Dengue kasi yake ya kusambaa jijini Dar es Salaam imeongezeka, na kuwataka wakazi wa jiji hilo kuchukua tahadhari.

Aidha, ametaja sehemu zinazo ongoza kwa kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa Dengue ikiwemo Wilaya ya Ubungo, Kinondoni na Ilala.

Amewataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kusafisha mazingira yanayo wazunguka ili kuondoa mazalia ya mbu wanaoeneza ugonjwa wa Dengue.

Dk. Ndungule amewataka Wananchi kufika hospitalini na katika vituo vya afya mapema pindi wanapo ona mabadiliko ya afya zao, ili wafanyiwe uchunguzi wa kitabibu, huku akisisitiza kwamba ugonjwa huo unapimwa bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!