Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watia nia wafutiwa mishahara
Habari za Siasa

Watia nia wafutiwa mishahara

Spread the love

SERIKALI imeagiza kwamba, watumishi wa umma waliotia nia ya kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa, wasilipwe mishahara yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Barua hiyo imetolewa na Ofisi ya Msajili wa Hazina tarehe 21 Julai 2020, likiwataka wakurugenzi na wakuu wote wa taasisi kuhakikisha, watumishi hao hawalipwi mishahara hiyo kuanzia Julai 2020.   

Neema Msonda, Msajili wa Hazina pia amewataka wakuu wa taasisi hizo kuandaa na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maelekezo hayo ifikapo tarehe 25 Julai 2020.

“Maelekezo haya ya kutolipa mshahara wa mwezi Julai, yanawahusu watumishi waliopatiwa vibali/ruhusa na waajiri wao pamoja na watumishi waliogombea bila vibali kutoka kwa waajiri wao au kupitia mamlaka stahiki,” imeeleza barua hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!