Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watanzania watahadharishwa na Corona
Afya

Watanzania watahadharishwa na Corona

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetahadharisha wananchi wake, juu ya hatari ya ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na mlipuko wa Virusi  vya Corona, unaotikisa dunia hivi sasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 29 Februari 2020, Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, amewataka Watanzania kuepuka vitendo vinavyoweza pelekea maambukizi ya ugonjwa huo.

Waziri Ummy amewataka Watanzania, kukwepa, kupeana mikono,  kukumbatiana na kupigana mabusu, katika kipindi hiki ambacho mlipuko huo umeshika kasi.

“Katika kipindi hiki ambacho kuna tishio la ugonjwa wa Corona, ninawataka wananchi kujizuia kupeana mikono, kukumbatiana na kubusiana hili linaweza kuwa gumu kwa Watanzania ila lazima niliseme,” amesema Waziri Ummy.

Wakati huo huo, Waziri Ummy  ametoa siku tatu kwa kila Mkoa nchini, kuwasilisha jina la kituo maalumu,  kilichotengwa kwa ajili ya kuhudumia washukiwa au wagonjwa wa Covid-19.

Hadi sasa virusi hivyo vimesambaa zaidi ya nchi 50 duniani, na kuuwa maelfu ya watu. Huku nchi ya China ikiwa mhanga mkubwa wa ugonjwa huo.

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema Tanzania haina mgonjwa wa Covid-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!