Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania wapewa somo hati ya kusafiria
Habari Mchanganyiko

Watanzania wapewa somo hati ya kusafiria

Spread the love

IDARA ya Uhamiaji imesema hati ya kusafiria ni haki ya kila Mtanzania ambaye anakidhi vigezo vya kuimiliki na inatolewa na serikali siyo matapeli wa mitaani, anaandikaMwandishi wetu.

Kauli hiyo imetolewa na Ofisa Uhamiaji mkoa wa Dodoma, Peter Kundy, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya maonesho ya wakulima na wafugaji nanenane kanda ya kati yaliyofanyika  kwenye viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma.

Kundy amesema kuwa licha ya kuwa hati ya kusafiria ni haki ya kila Mtanzania, lakini mwananchi huyo ni lazima awe amekidhi vigezo vinavyohitajika kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Hata hivyo, amesema wananchi wanatakiwa kuwa makini na baadhi ya watu ambao ni matapeli wanaojifanya kuwa ni maofisa Uhamiaji wakati ni uongo.

Amesema hati za kusafiria hupatikana katika ofisi za idara ya uhamiaji baada ya mtu  kujaza fomu maalumu ambazo kwa sasa zinapatikana nchi nzima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!