Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Watalaam wakuna vichwa usugu wa dawa
Habari Mchanganyiko

Watalaam wakuna vichwa usugu wa dawa

Duka la dawa
Spread the love

CHAMA cha Wafamasia nchini (PST), kimeiomba serikali kusaidiana nacho ili kuhakikisha wanatokomeza tatizo la usugu wa dawa za binadamu, anaandika Mwandishi wetu.

PST kimesema tatizo hilo husababisha vifo na kwamba wakishirikiana na serikali wanaweza kuliondoa.
Hayo yameelezwa na  Katibu mkuu wa chama hicho, Geofrey  Yambayamba katika shule ya wasichana Msalato iliyopo Dodoma wakati wa kuhitimisha kampeni ya mwezi mmoja ya kutoa elimu ya madhara yanayotokana na usugu wa dawa.

Amesema kundi linalokabiliwa na tatizo la usugu wa dawa ni pamoja na wanafunzi wa sekondari kwa kuwa hawamalizi dozi wanapoandikiwa na daktari.

“Wanafunzi wengi wa shule za sekondari ni miongoni mwa watu waliopo hatarini kupatwa na usugu wa dawa kutokana na ukweli kwamba mara nyingi huwa hawamalizi dozi na kusababisha magonjwa kujirudia rudia”alisema.

Amewataka wanafunzi hao kufikisha elimu kwa jamii kuhusu matumizi sahihi ya dawa na kwamba kila mtu anatakiwa kutumia dawa ambazo hazijaisha muda wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!