Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watakiwa kutotumia nafaka kutengeneza pombe
Habari Mchanganyiko

Watakiwa kutotumia nafaka kutengeneza pombe

Mwananchi akianika ulezi kwa ajili ya kutengenezea pombe
Spread the love

MUSTAFA Rajabu Sheikh wa Mkoa wa Dodoma na Kadhi wa Mkoa huo amewaasa Watanzania kutotumia nafaka kama mahindi na mtama kwaajili ya kutengeneza pombe za kienyeji ilihali kuna uhaba wa chakula uliosababishwa kuchelewa kwa mvua, anaandika Dany Tibason.

Sheikh Mustafa ameyasema hayo alipokuwa ikitoa mawaidha katika ibada ya  leo Ijumaa katika msikiti wa Gadafi mjini hapa.

Mbali na hilo pia, sheikh huyo amewataka wananchi kutumia vyema mvua zinazonyesha kwa kupanda mazao ya muda mfupi na yasiyohitaji mvua kubwa.

“Viongozi wa dini mbalimbali tulifunga na kuomba ili mvua iweze kunyesha, na maombi hayo yamejibiwa kwani mvua zimeanza kunyesha hivyo ni wajibu wa Watanzania kutumia mvua hizo kwaajili ya kupanda mazao ya muda mfupi.

“Wakulima waachane na tabia ya kuuza mazao yakiwa shambani na badala yake wavute subira ili waweze kuvuna na wauze kwa vipimo ambavyo vinastahili,” amesema.

Katika hatua nyingine Sheikh Mustafa amewataka watawala hapa nchini kuhakikisha wanasimamia haki katika utendaji wao wa kila siku.

“Vitabu vyote vitakatifu vinahimiza utoaji wa haki hivyo ni lazima viongozi wote wenye mamlaka wasimamie haki bila kuwaonea wenzao au kuwatengenezea majungu kwa nia ya kuwakomoa.

“Vyombo vyote vinavyohusika katika utoaji haki lazima vitende haki, mabaraza yote ya maamuzi lazima yasimamie haki kwani haki ndiyo inaweza kuliweka Taifa katika hali ya usalama zaidi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!