Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wastaafu waililia Serikali ya JPM
Habari Mchanganyiko

Wastaafu waililia Serikali ya JPM

Spread the love

ZAIDI ya wastaafu 300 kutoka wilaya za Nyamagana na Ilemela Mkoani Mwanza, wameilalamikia Serikali kwa kuwakata makato makubwa ya pensheni zao za kila miezi mitatu kwani hayaendani na hali halisi ya maisha, anaandika Moses Mseti.

Wakizungumza leo katika zoezi la kufanyiwa uhakiki, linalofanywa na Wizara ya Fedha na Mipango wamedai kwamba licha ya makato hayo makubwa bado pensheni wanayolipwa kwa mwezi haizidi Sh. 80,000/= na 90,000/=

“Kiasi cha fedha tunacholipwa, hakiendani na hali ya maisha ya sasa. Serikali inapaswa kuangalia namna bora ya kutuongezea pensheni za kila mwezi au baada ya miezi mitatu ili kuendana na hali halisi ya maisha,” amesema Salome Sabula, mmoja kati ya wastaafu hao.

Kwa upande wake mstaafu mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Elizabeth Sylvester amesema, “mimi watoto wangu nimesomesha lakini mpaka sasa baada ya Serikali kusitisha ajira wapo tu nyumbai bado naendelea kuwasomesha wengine, sasa Sh. 80, 000/= tunazolipwa kwa mwezi zitasaidia nini?”

Wamesema kipindi walipostaafu mwaka 1990, walilipwa Sh. milioni 4.4 tu huku walimuomba Rais John Magufuli, kuwaangalia wastaafu wa zamani ili waongezewe fedha ili kukabiliana na makali ya maisha.

Stanslaus Mpembe, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha na Mipango amesema lengo la uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na wizara hiyo kwenye mikoa mitano ya Kanda ya ziwa unalenga kubaini wastaafu sahihi wanaopaswa kulipwa na serikali.

“Pamoja na kuhakiki wastaafu hao pia tunalenga kuondoa malalamiko na changamoto za wastaafu zilizokuwepo kwa muda mrefu na tunawahimiza wajitokeza kuhakikiwa kabla ya zoezi hilo kukamilika mnamo tarehe 13 Januari mwaka huu,” amesema Mpembe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!