Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wapinzani DRC kumtikisa Kabila
Kimataifa

Wapinzani DRC kumtikisa Kabila

Jean-Pierre Bemba
Spread the love

HATUA ya Mahakama ya Juu nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kutangaza kuwa, mgombea wa chama kikuu cha upinzani-MCL- Jean-Pierre Bemba hana sifa ya nafasi ya urais, inapeleka taifa hilo kwenye maandamano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tayari chama kikuu cha upinzani MCL nchini humo kinajiandaa kufanya maandamano kupinga kauli hiyo pamoja na uchaguzi mkuu ujao. Bemba ameondolewa kwenye orodha ya wagombea urais wan chi hiyo kwa madai ya kukosekana ushahidi wa kutosha pia mahakama kukosa imani na upande wa ushahidi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai.

MCL kinaendelea na vikao vya ndani ambapo taarifa ya awali imeeleza kuwa, watatangaza tarehe ya maandamano hayo na kwamba, uamuzi wa mahakama ya juu ni wa hovyo.

Pamoja na hivyo MCL inaituhumu tume ya uchaguzi ya nchi hiyo pamoja na mahakama nchini kuwa vinaendesha shughuli zake kwa kuegemea upande wa chama tawala.

Swali ni kuwa, je chama cha MCL kitaunga mkono mgombea mwingine kutoka kambi ya upinzani ambaye ana fursa ya kugombea nafasi hiyo au watabadili mwelekeo na kushughulika na mchakato mzima? Haijafahamika.

Bemba kwa sasa yuko mjini Brussels, alirejea mjini Kinshasa Agosti, lakini kurejea kwake tena nchini humo kumeahirishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!