Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wapiga dili CCM kuhenyeshwa
Habari za SiasaTangulizi

Wapiga dili CCM kuhenyeshwa

Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dodoma
Spread the love

ROBERT Mwinje (39) na  Nyemo Malendaa(20), wote makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Dodoma wanatarajiwa kupandishwa kizimbani muda wowote kutoka sasa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwinje aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini na Malendaa, mhudumu wa ofisi hiyo wanakabiliwa na makosa ya kula njama, kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo za uteuzi wa waombaji uongozi ndani ya chama hicho.

Sosthenes Kibwengo, Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Dodoma amesema Mwinje na Nyemo waligushi barua ya uteuzi wa waomba uongozi ndani ya chama hicho.

Pia walidai imetolewa na uongozi wa chama wilaya ya Dodoma, wakaikabidhi kwa mwanachama mmoja kwa hatua huku wakifahamu kwamba ni uongo.

Mwinje aliondolewa katika nafasi yake hiyo ya uenyekiti hivi karibuni na kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika jijini Mwanza. Kikao hicho kiliongozwa na Dk.John Magufuli, Mwenyekiti wa chama Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!