Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waombewe wapate laana – Rais Magufuli
Habari za Siasa

Waombewe wapate laana – Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

UKOSEFU wa maadili, tabia ya kuchelewesha kesi kwa makusudi na kuendekeza rushwa katika Mahakama za Tanzania, kunamkwaza Rais John Magufuli. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea). 

Akizungumza kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria, jijini Dar es Salaam leo tarehe 6 Februari 2020, Rais Magufuli ameshauri viongozi wa dini wawaombee wanaofanya vitendo hivyo wapate laana.

“Niwaombe viongozi wa dini, kaliombeeni sana suala hili ili wale wanaochelewesha kwa makusudi, wakapate laana ili Mungu akaanze kuwaadhibu wao, kabla ya wale waliowaweka mahabusu,” amesema Rais Magufuli.

Amesema, kuna tatizo la kukosekana kwa maadili ikiwemo kubambikia watu kesi, jambo ambali linavuruga taswira ya mahakama, na kwamba kila mmoja anawajibika kukosoa dosari hizo.

“Kuna matatizo ya kukosekana kwa maadili, ikiwemo kuendeleza vitendo vya rusha kwa kubambikiza kesi kama nilivyosema.

 Tuna wajibu wa kukosoa hizo dosari sisi wote kwa pamoja na kumtanguliza Mungu ili watu wasikosee,” amesema.

Ameeleza changamoto nyingize inayoikumba Mahakama za Tanzania, nikuendelea kukithiri kwa migogoro ya ardhi, na kwamba waathirika wakubwa wamekuwa wanawake hususani wajane.

Amesema, amekuwa akifanya ziara maeneo mbalimbali ya nchi, miongoni mwa mambo makubwa anayokumbana nayo ni migogoro ya ardhi.

Hivyo, ameyataka Mabaraza ya Ardhi kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha haki inatendeka, huku akishuri kuundwa kwa timu maalum ya kushughulikia matatizo hayo.

Anasema, hana hakika kama Mabaraza ya Ardhi yanafanya kazi vizuri, na kwamba serikali inawezekana ilifanya makosa kuyaacha yakiwa huru.

“Lakini pale lawama zinapotokea, inanyooshewa kidole mahakama,” amesema huku akisema mabaraza hayo badala ya kuwa chini ya Wizara ya Ardhi, yawe chini ya mahakama ili yashughulikiwe vizuri.

“Kwenye Mabaraza ya Ardhi kuna kelele nyingi, wale watu kule wanapindua wanavyotaka, mimi nimekaa Wizara ya Ardhi, nafahamu,” amesema Rais Magufuli.

Pia kiongozi huyo wa nchi, ameipongeza mahakama kwa kufanya kazi nzuri na yenye mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

“Naipongeza sekta ya sheria na mahakama nchini kwa kupata mafanikio makubwa, ikiwemo kupungua kwa muda wa usikilizwaji wa kesi, kuimarisha matumizi ya TEHAMA pamoja na kuanzisha mahakama zinazotembea,amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

Regina Mkonde: CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!