Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewataka waombaji mikopo katika mwaka wa masomo 2018/2019 ambao fomu zao zina kasoro, kurekebisha kasoro hizo ndani ya siku saba kuanzia Septemba 24 hadi 30, 2018 ili wapangiwe mikopo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na HESLB, inaeleza kwamba zaidi ya waombaji 25,000 katika maombi ya mikopo 78,833 yaliyopokelewa Julai 31, 2018 , fomu zao zilibainika kuwa na upungufu wa nyaraka na uthibitisho wa kuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ya kupangiwa mikopo katikati ya mwezi Oktoba, mwaka huu.
HESLB imewataka waombaji hao kupitia majina yao kwenye orodha iliyowekwa katika tovuti ya bodi hiyo, kisha kuingia kwenye mtandao wa maombi ya mikopo ili kufanya masahihisho kwa kufuata hatua zilizowekwa na baada kukamilisha, waziwasilishe ndani ya muda uliopangwa bila kutuma tena kwa njia EMS .
“Kwa taarifa hii pia tunapenda kuwakumbusha waombaji wa mikopo ambao wamo katika orodha hiyo yenye upungufu wa taarifa kusoma kwa umakini na kurekebisha kasoro hizo ili waweze kupangiwa mikopo. Aidha tunawatahadharisha dhidi ya matapeli wanaoweza kutumia taarifa hiI kuwalaghai waombaji mikopo kuwa wanaweza kuwasaidia kupata mikopo. Tangazo maalum na mwongozo wa marekebisho vinapatikana katika tovuti hii,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Leave a comment