Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanne Chadema wachuana ubunge Kinondoni
Habari za Siasa

Wanne Chadema wachuana ubunge Kinondoni

Spread the love

WANACHAMA wanne wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamejitosa katika kinyang’anyiro cha kugombea Ubunge Kinondoni jijini Dar es Salaam katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Watia nia hao, leo Jumatatu tarehe 13 Julai 2020, wanapigiwa kura za maoni na wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo hilo ambalo kwa sasa mbunge anayemaliza muda wake ni Maulid Mtulia wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wanaochuana kwenye mbio hizo ni; Susan Lyimo, Mbunge Viti Maalum, Moza Ally, Makamu Mwenyekiti Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), Mbesi Mombeki na Rose Mushi, Diwani wa Viti Maalum.

Mchakato huo wa kura za maoni unaoendelea katika Ukumbi wa Garden, Mwananyamala jijini Dar es Salaam, unasimamiwa na Kubra Abdallah.

Kura za maoni ndani ya Chadema kwa ajili ya kupata wagombea ubunge, zimeanza baada ya shughuli ya uchukuaji na urudishaji fomu  kufungwa tarehe 10 Julai 2020.

Kwa sasa wajumbe wanaendelea kupiga kura.

Baada ya shughuli ya kura za maoni kufungwa, Kamati Kuu ya Chadema itaketi tarehe 30 hadi 31 Julai 2020, kwa ajili ya kuteua wagombea ubunge wa chama hicho, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.

Kwa mujibu ya ratiba iliyotolewa na Chadema, kura za maoni kwa wabunge zimeanza leo hadi tarehe 17 Julai 202

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!